burudan

Uchunguzi wa ajali ya EgyptAir utachukua muda

Ndege hiyo iliwauwa abiri wote 66 waliokuwemo.
Rais wa Misri Abdel Fattah al-Sisi, anasema kuwa kila kitu kinachoaminiwa kusababisa ajali, kinasalia jinsi kilivyo kuhusiana na ajali ya ndege ya EgyptAir, iliyoanguka siku ya Alhamisi.

Bwana Al-Sisi amesema pia kuwa uchunguzi utachukua muda mrefu kukamilika huku akiviomba vyombo vya habari kujiepusha kueneza uvumi kuhusiana na kiini cha ajali hiyo.
Ndege hiyo iliwauwa abiri wote 66 waliokuwemo.
Hapo jana Jumamosi, wachunguzi wa Misri walisema ni mapema mno kufikia hatma ya kilichosababisha ajali hiyo kwani uchunguzi wa data bado haujakamilika.

Kikosi kinachoendelea na msako kinaendelea kutafuta mabaki ya ndege hiyo pamoja na kisanduku cha kuhifadhi mawasiliano ya ndege.

Geen opmerkingen:

Een reactie posten

KBSBLOG Designed by Templateism.com Copyright © 2014

Thema-afbeeldingen van Bim. Mogelijk gemaakt door Blogger.
Published By Gooyaabi Templates