burudan

MJUE LIONEL MESSI

Lionel Messi

Lionel Andrés Messi (amezaliwa Rosario, Argentina, 24 Juni 1987) ni mchezaji wa mpira wa miguu kutoka nchi ya Argentina.
Tangu mwaka 2003 amechezea klabu ya Fc Barcelona (Hispania).
Maisha 
Alizaliwa akiwa njiti (yaani kabla ya miezi 9), akachukuliwa na Barcelona akiwa na umri wa miaka nane (8). Akalelewa ndani klabu ya kukuzia vipaji ya Barcelona inayofahamika kama Katalunya (Catalan), akichezea timu ya watoto akiwa ndiye mwenye umri mdogo zaidi.
Alianza kuchezea timu ya wakubwa mwaka 2003, akiwa anavaa namba 19 mgongoni,wakati namba 10 ilikuwa inavaliwa na Mbrazili Ronaldinho.
Aliaanza kuingia kwenye historia ya soka duniani mwaka 2009 baada ya kuiwezesha Barcelona kutwaa ubingwa wa klabu bingwa Ulaya (UEFA), na FIFA kumpa tuzo ya mwanasoka bora wa dunia.
Aliendeleza historia na kuweka historia ya pekee duniani kwa kuchukua tuzo hiyo mara 4 mfululizo.

Sifa za Lionel Messi baada ya kushindia taji la Ballon D'or

Hatua ya Lionel Messi kunyakua taji la mchezaji bora katika mchezo wa soka duniani kwa mara ya tano na kuweka historia ya kuwa mchezaji wa kwanza kuwahi kufikia kiwango hicho, inaweka wazi mafanikio ya mshambuliaji huyu matata.
Messi mwenye umri wa miaka 28 raia wa Argentina, alianza kuichezea Barcelona mwaka 2001 akiwa kijana chipukizi na hadi sasa bado anakipiga na klabu hiyo.
Kuendelea kuichezea Barcelona kumemjenga na kumfanya kuwa na nidhamu nje ya ndani ya uwanja.
Unyenyekevu wa Messi pia umemsaidia katika uchezaji wake na hata alipotangazwa mshindi alionekana mtulivu na hata kuwapa mkono wenzake, Neyma na Christiano RonaldoMessi 
amekuwa mfungaji bora katika ligi kuu nchini Uhispania La Liga mara 3, msimu wa mwaka 2009-2010 alifunga mabao 34, 2011-2012 akafunga mabao 50 na msimu wa mwaka 2012-2013 alifunga mabao 46.
Amewahi pia kuongoza katika ufungaji wa mabao katika michuano ya klabu bingwa mara tano, mwaka 2008-2009 alifunga mabao 9, 2009-210 mabao 8, 2010-2011 mabao 12, mwaka 2011-2012 mabao 14 na mwaka 2014-2015 mabao 10.
Messi ameisaidia klabu yake kushinda mataji yafuatayo:
·         Klabu bingwa barani Ulaya mara 4 : 2005-06, 2008-09, 2010-11, 2014-15
·         Kombe la dunia kwa vlabu (3): 2009, 2011, 2015
·         Taji la Super Cup barani Ulaya (3): 2009, 2011, 2015
·         Ligi kuu ya soka nchini Uhispania (7): 2004-05, 2005-06, 2008-09, 2009-10, 2010-11, 2012-13, 2014-15


Rekodi zake mpya hizi hapa                                             Lionel Messi amefunga magoli 15 katika mechi 13 za UEFA Ligi ya Mabingwa dhidi ya timu za Uingereza.

Goli la kwanza la kwenye mchezo huo lilikuwa ni goli la 100 kwa safu ya MSN kwenye mashindano yote kwa mwaka 2016.
Messi kwa sasa anaongoza orodha ya wafungaji katika viwanja vya nyumbani kwenye michuano ya Ulaya akiwa mefunga magoli 50


Geen opmerkingen:

Een reactie posten

KBSBLOG Designed by Templateism.com Copyright © 2014

Thema-afbeeldingen van Bim. Mogelijk gemaakt door Blogger.
Published By Gooyaabi Templates