burudan

Msichana wa Chibok apatikana Nigeria


Wanaharakati nchini Nigeria wanasema kuwa mmoja wa wasichana wa shule wa Chibok, waliotekwa nyara na kundi la Boko Haram amepatikana, akiwa ndiye mtu wa kwanza kukolewa kwa zaidi ya miaka miwili.
Zaidi ya wasichana 200 walitekwa nyara na wanamgambo wa Boko Haram kutoka mji ulio Kaskazini Mashariki mwa Nigeria zaidi ya miaka miwili iliyopita.
Mwanaharakati Hauwa Abdu aliiambia BBC kuwa, msichana huyo alipatikana siku ya Jumanne jioni na kundi moja la kuweka ulinzi baada ya makabiliano na watu wanaokisiwa kuwa wapiganaji wa Boko Haram.

Kiongozi mmoja wa kijamii alisema kuwa msichana huyo alikuwa na mtoto na wote wamekabidhiwa jeshi la Nigeria katika mji wa Damboa.

Geen opmerkingen:

Een reactie posten

KBSBLOG Designed by Templateism.com Copyright © 2014

Thema-afbeeldingen van Bim. Mogelijk gemaakt door Blogger.
Published By Gooyaabi Templates