burudan

Semenya ashinda mbio za Diamond League

Semenya anatarajiwa kushinda dhahabu Olimpiki
Mwanariadha Caster Semenya kutoka Afrika Kusini ameshinda mbio za 800m za wanawake katika mashindano ya Diamond League yaliyofanyika Rabat, Morocco.

Hii ni mara ya kwanza kwa msururu wa mashindano hayo kuandaliwa barani Afrika.
Semenya, 25, alifanyiwa uchunguzi wa kubaini jinsia yake kamili baada yake kushinda dhahabu mashindano ya ubingwa wa riadha ya mwaka 2009.
Alimaliza mbio hizo za mjini Rabat katika muda sekunde 56.64, muda bora zaidi mwaka huu.
Anapigiwa upatu kushinda dhahabu kwenye Michezo ya Olimpiki ya mwaka huu mjini Rio 2016, ambapo anapanga pia kukimbia mbio za 400m.

Mwingereza Lynsey Sharp alimaliza wa tano.

Geen opmerkingen:

Een reactie posten

KBSBLOG Designed by Templateism.com Copyright © 2014

Thema-afbeeldingen van Bim. Mogelijk gemaakt door Blogger.
Published By Gooyaabi Templates