burudan

Rooney kuwacha safu ya mashambulizi


Mshambuliaji wa klabu ya Manchester United na Uingereza Wayne Rooney amesema kuwa huenda akaanza kucheza katika safu ya kati katika siku za usoni baada kucheza vyema katika safu hiyo dhidi ya Bournemouth katika uwanja wa Old Trafford.
Katika mechi hiyo ya kufunga lgi ya uingereza,man United ilipata ushindi wa maba0 3-1 .
Nahodha huyo wa kikosi cha Uingereza alifunga bao la kwanza kabla ya kumpatia pasi nzuri Ashley young kwa bao la tatu.

''Mara nyengine unafaa kuamua katika kazi yako na kwa sasa ni bora mimi kucheza katika safu ya kati'',alisema.
''Inaweza kuwa tofauti kwa timu ya Uingereza ambapo ninaweza kuwa mshambuliaji, lakini pengine msimu ujao huenda nikacheza katika safu hiyo''

Geen opmerkingen:

Een reactie posten

KBSBLOG Designed by Templateism.com Copyright © 2014

Thema-afbeeldingen van Bim. Mogelijk gemaakt door Blogger.
Published By Gooyaabi Templates