burudan

Jide; Ray C anahitaji marafiki sahihi.

STAA wa muziki wa Bongo Fleva, Judith Wambura ‘Lady Jaydee’ a.k.a Jide, amesema msanii mwenzake, Rehema Chalamila, anahitaji marafiki sahihi ambao watamsaidia katika kipindi hiki kigumu.

Ray C ambaye amewahi kujihusisha na madawa ya kulevya, kwa sasa ameripotiwa kurejea kwenye matumizi hayo huku mara kadhaa ikiripotiwa kuwa mrembo huyo aliyekimbiza na Kibao cha Na Wewe Milele, amerejea kwenye utumwa huo wa madawa hayo ambayo ni hatari.

Jide alizungumza hayo Ijumaa iliyopita alipokuwa akizindua kichupa chake cha Ndi Ndi Ndi kwenye Kipindi cha Friday Night Live kinachorushwa na East Africa Television na Radio. Alisema alikuwa hajakutana muda mrefu na Ray C kabla ya juzikati alipokwenda kumsalimia nyumbani kwake.

Geen opmerkingen:

Een reactie posten

KBSBLOG Designed by Templateism.com Copyright © 2014

Thema-afbeeldingen van Bim. Mogelijk gemaakt door Blogger.
Published By Gooyaabi Templates