Klabu ya soka ya crystal Palace
imetinga hatua ya Fainali ya FA CUP baada ya kuifunga Watford United Bao
2-1 kwenye Nusu Fainali.
Hadi Mapumziko Palace walikuwa mbele kwa Bao 1-0 lililofungwa na Yannick Bolasie.
Kipindi cha Pili, Watford walimudu kusawazisha kupitia Deeney lakini Dakika 6 tu baadae Connor Wickham akafunga Bao la Pili na la ushindi kwa Palace.
Fainali Michuano hii itachezwa Mei 21 hapo hapo katika dimba laaWembley.



Geen opmerkingen:
Een reactie posten