![]() |
Marekani imeonya kwamba michuano ya soka ya Euro 2016 itakayofanyika nchini Ufaransa mwezi ujao huenda ikalengwa na wapiganaji.
Kinyang'anyiro hicho kitaandaliwa kuanzia mwezi Juni 10 hadi tarehe 12 Julai katika maeneo tofauti.
France imewekwa katika hali ya tahadhari kufuatia shambulio la Islamic State mjini Paris.
![]() |
Timu ya Wales |
Mshambulio hayo yanaweza kulenga maeneo ya kitalii,migahawa,vituo vya kibiashara na uchukuzi.
Geen opmerkingen:
Een reactie posten