Lulu Michael na Gigy Money Wacharuana....
MASTAA wawili wa filamu, Elizabeth Michael ‘Lulu’ na Gift Stanford ‘Gigy Money’ wamejikuta wakiingia kwenye mtifuano mkali baada ya kutoleana maneno machafu.
Chanzo makini kilieleza kuwa ishu ilianzia kwa Gigy ambaye alisema mwanadada Lulu hajui kuvaa anavaa matangazo, hii ni baada ya kuulizwa na kituo kimoja cha runinga kwamba ataje mastaa kumi wanaojua kuvaa ambapo Lulu alimjibu kupitia ukurasa wake wa Mtandao wa Kijamii wa Instagram kuwa bora asijue kuvaa lakini hawezi kuvaa matambara kama yeye.
“Yaani Gigy alikasirishwa sana na kitendo cha Lulu kumwambia anavaa matambara alijikuta akipaniki na yeye akaendelea kushilikilia msimamo kwamba anavaa nguo za matangazo hivyo ni bora yeye anayevaa matambara anayonunua mwenyewe kuliko yeye,” kilisema chanzo.
Baada ya kupata maelezo ya chanzo, paparazi wetu alimtafuta Gigy na kumuuliza kulikoni ambapo alisema amekasirishwa sana na kitendo cha Lulu kumwambia anavaa matambara wakati yeye alizungumza kama anavyoona kwani mavazi anayovaa hayaendani na mazingira.
“Matambara ni ya kwangu na haya ni maisha yangu siyo yeye anayevaa nguo za matangazo eti anajiona naye anavaa maana naona Lulu ameunda na kampeni na makundi kwa ajili ya kunishambulia, mimi ni jeshi la mtu mmoja hawaniwezi,” alisema Gigy Money.
Ili kuleta mzani wa habari, gazeti hili lilimtafuta Lulu lakini mpaka linaenda mtamboni simu yake ilikuwa ikiita tu bila kupokelewa.
Abonneren op:
Reacties posten (Atom)
ALIKIBA NCHINI UJERUMAN
Follow us on facebook
Popular Posts
-
Leo tutaongelea kuhusu furaha na afya katika michezo mbalimbali ndani ya jamii. Kuna aina za michezo nyingi sana katika jamii hivyo basi ...
-
Miongozo mipya iliyotolewa nchini Marekani inapendekeza wanawake wajawazito kufanya mazoezi mepesi karibu siku zote za ujauzito. Tofauti...
-
Mchezaji akicheza mpira karibu na shimoni kwa fimbo la "putter" Mchezaji akicheza mpira karibu na shimoni kwa fimb...
-
MUONEKANO WA HALISI WA BAO NA KETE ZAKE Habari ndugu msomaji wa makala hii ya Ielewe Michezo leo tutakuwa tukiangazia juu ya m...
-
Lionel Messi Lionel Andrés Messi (amezaliwa Rosario, Argentina , 24 Juni 1987 ) ni mchezaji wa mpira wa miguu kutoka ...
-
hiki ni kibao cha chuo cha uandishi wa habari na utangazaji arusha <AJTC> hili ni jengo la utawala katika chuo cha uan...
-
Syria imetangaza usitishaji wa mapigano wa muda mfupi karibu na Damascus na katika jimbo moja lakini haikutaja juu ya mapigano katika me...
-
1. Ni sayari ambayo kila baada ya miaka 3600 huingia katika solar system yetu na huikaribia dunia ila haitaigonga dunia. 2. Ni sayari am...
-
Nchi inaweza kuwa maskini zaidi duniani kama wana Pato duni la Asili , Kuna rasilimali kidogo, ukosefu wa ajira na maendeleo ...
-
Aliyekuwa mke wa rapa Wiz Khalifa ‘Amber Rose’ amejitamba hivi karibu akiwa na mp...
Geen opmerkingen:
Een reactie posten