Mkurugenzi
Mtendaji wa Halmashauri ya Singida, Simion Mumbee amesimamishwa kazi
baada ya kudaiwa kutoa taarifa za uongo kuhusu watumishi hewa.
Katika taarifa hiyo, Mumbee anadai watumishi hewa 19 waliogundulika
kwenye halmashauri hiyo hawajaisababishia hasara Serikali jambo
linalodaiwa kuwa si kweli.
Akizungumza jana kwenye ufunguzi wa kikao cha maendeleo mkoani humo,
Mkuu wa Mkoa wa Singida, Mathew Mtigumwe alisema anamsimamisha kazi
mkurugenzi huyo ili kupisha uchunguzi.
“Nilipotuma tume kufuatilia suala la watumishi hewa katika Halmashauri
ya Wilaya ya Singida, ilibaini wapo na wameisababishia Serikali hasara
ya zaidi ya Sh125 milioni,” alisema Mtigumwe.
Alisema taarifa ya Mumbee ililenga kuidanganya Serikali. Mtigumwe
alimuagiza Katibu Tawala wa Mkoa, Dk Angela Lutambi kumuandikia barua ya
kumsimamisha kazi mara moja.
Mtigumwe alisema hana nafasi ya kufanya kazi na watumishi wa aina ya Mumbee.
Wakati huo huo; Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma, Said Mwambungu amemsimamisha
kazi Ofisa Utumishi wa Halmashauri ya Wilaya ya Songea, Philbert Mtweve
kwa tuhuma za kuwalipa mishahara watumishi hewa wanane na kuisababishia
Serikali hasara ya Sh27 milioni.
Abonneren op:
Reacties posten (Atom)
ALIKIBA NCHINI UJERUMAN
Follow us on facebook
Popular Posts
-
Leo tutaongelea kuhusu furaha na afya katika michezo mbalimbali ndani ya jamii. Kuna aina za michezo nyingi sana katika jamii hivyo basi ...
-
Miongozo mipya iliyotolewa nchini Marekani inapendekeza wanawake wajawazito kufanya mazoezi mepesi karibu siku zote za ujauzito. Tofauti...
-
MUONEKANO WA HALISI WA BAO NA KETE ZAKE Habari ndugu msomaji wa makala hii ya Ielewe Michezo leo tutakuwa tukiangazia juu ya m...
-
Mchezaji akicheza mpira karibu na shimoni kwa fimbo la "putter" Mchezaji akicheza mpira karibu na shimoni kwa fimb...
-
1. Ni sayari ambayo kila baada ya miaka 3600 huingia katika solar system yetu na huikaribia dunia ila haitaigonga dunia. 2. Ni sayari am...
-
Lionel Messi Lionel Andrés Messi (amezaliwa Rosario, Argentina , 24 Juni 1987 ) ni mchezaji wa mpira wa miguu kutoka ...
-
Waziri wa michezo Fikile Mbalula Afrika Kusini haitaandaa mashindano ya Raga, Kriketi, Riadha na Netiboli baada ya se...
-
A man who str!pped n@ked and entered a lion enclosure in a Chilean zoo has survived the incident, but the lions were killed. S...
-
hiki ni kibao cha chuo cha uandishi wa habari na utangazaji arusha <AJTC> hili ni jengo la utawala katika chuo cha uan...



Geen opmerkingen:
Een reactie posten