Wapiganaji wa kundi la Islamic State wameshambulia mgahawa mmoja unaotembelewa na mashabiki wa Real Madrid na kuwaua watu 12.
Washambuliaji hao walitoroka na saa chache baadaye huku mmoja wao akajilipua alipokamatwa na wapiganaji wa Shia,na kuwaua wanne wao.
Baada ya kukiri kutekeleza shambulio hilo kundi la wapiganaji wa Islamic State lilisema kuwa shambulio hilo liliwalenga wapiganaji na halikuhusishwa na Real Madrid.
''Klabu hiyo ilisikitishwa sana na shambulio hilo na kutuma rambirambi kwa familia na marafiki wa waathiriwa'',ilisema taarifa.
Geen opmerkingen:
Een reactie posten