Wapiganaji wa Kiislamu wa Somalia, Al Shabab wanasema wamewauwa wanajeshi wa serikali zaidi ya 30.
Wenyeji wa kijiji hicho wamethibitishia BBC, kwamba kijiji chao kinadhibitiwa tena na wanamgambo wa Al Shabab.
Kwengineko nchini Somalia, watu kama watatu waliuwawa, kwenye shambulio la bomu, katika soko la mifugo huko Qoryoolay, inavoelekea shambulizi hilo lililengwa maafisa wa kukusanya kodi wa serikali.
Geen opmerkingen:
Een reactie posten