WHO: Ugonjwa wa kisukari waongezeka duniani
Shirika la afya duniani WHO limesema Idadi ya watu wanaokadiriwa kuishi
na ugonjwa wa kisukari imeongezeka mara nne zaidi ndani ya miaka 35
iliyopita.
Katika ripoti yake ya kwanza juu ya ugonjwa huo wa kisukari shirika hilo la WHO limesema mwaka wa 2012 ugonjwa huo uliripotiwa kusababisha vifo vya watu milioni 1.5 duniani, huku vifo vinavyotokana na kupanda kwa viwango vya sukari mwilini vinavyofungamanishwa na kisukari vikiripotiwa kufikia watu milioni 2.2 mwaka huo huo wa 2012.
"Ugonjwa wa kisukari ndio moja ya ugonjwa unaoua watu wengi duniani kwa sasa," alisema Etienne Krug, anayeongoza kitengo kinachoshughulika na uitikiaji wa ugonjwa huo katika shirika la WHO.
Aidha eneo lililoathirika sana kwa kuwa na visa milioni 131 vya ugonjwa huo mwaka 2014 ni eneo la pasifiki ya Magharibi linalojumilisha mataifa kama Japan na China, eneo la pili ambalo ni Kusini Mashariki mwa Asia linalojumuisha maeneo yaliyo na idadi kubwa ya watu kama India na Indonesia wana visa milioni 96 vya ugonjwa huo.
Huku Ulaya na Amerika wakishika nafasi za tatu na nne katika orodha hiyo wakiwa na visa milioni 64 na milioni 62 vya ugonjwa wa kisukari.
Ugonjwa huo umegawika katika aina mbilii. Hakuna njia ya kukwepa aina ya kwanza ambapo inatokea pale kongosho au Pancrease kwa lugha ya kingereza inaposhindwa kutengeneza homoni ya insulin inayodhibiti viwango vya sukari kwenye damu, na wale wanaoishi na aina ya pili ya ugonjwa huo inafungamanishwa na uzito kupita kiasi, namna mtu anavyoishi, na hii inaweza kuepukika kwa watu wazima na watoto kuzingatia lishe bora na kufanya mazoezi.
WHO inapendekeza watu wazima kuanzia miaka 18 hadi 65 kufanya mazoezi ya angalau dakika 150 kwa wiki ikiwa ni pamoja na shughuli za kimwili kama vile kukimbia na kutembea.
Geen opmerkingen:
Een reactie posten